Breaking News

NEWS simu Feki Zote Kufungiwa, Ingia Hapa Kuijua Ya Kwako


Aina mbalimbali za simu.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)  imetoa maelekezo ya kuangalia  simu yako kama ni feki  au origino.
Ili kujua kama simu ni origino au feki unachotakiwa  ni kubonyeza *#06# ili upate namba ya IMEI, na kisha hiyo IMEI namba  uitume kwenda namba 15090 ambapo utapokea ujumbe utakaokufahamisha kama simu  yako ni feki au origino. Kumbuka kutuma ujumbe huo ni bure kabisa.
Mamlaka  hiyo imetoa tangazo la kuwataka watumiaji wa simu kujiridhisha kama simu zao ni origino kwa kuwa inatarajia kuzifungia simu zote feki  ifikapo  17.6.2016.
TCRA ndicho chombo kilichoanzishwa kisheria kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji nchini  hivyo ni jukumu lako kuchukua hatua mapema kabla simu  yako haijafungiwa

No comments