NEWS KUTOKA VIKINDU: Majambazi zaidi ya 10 wakamatwa, wakiwemo askari na Kanali Mstaafu
UPDATE KUTOKA VIKINDU: Wamekamatwa jumla ya majambazi 14 na wengi wao ni askari wastaafu.
- Kiongozi wao ni Kanali Mstaafu wa Jeshi.
Zaidi, soma
Imetokea usiku huu Mkuranga. Askari wazingira nyumba ambayo walikuwa wanafanya uchunguzi baada ya mauaji ya polisi Mbande.
Radio WAPO.
========
UPDATES;
> Mapigano makali yanaendelea kati ya polisi na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi eneo la Vikindu, wilaya ya Mkuranga, mkoa wa Pwani.
> Timu ya Mwananchi iliyo eneo la tukio imeshuhudia magari ya polisi (difenda) zaidi ya 16 yakifika eneo la tukio huku polisi wakiwa wameshika silaha zao kwa umakini mkubwa.
> Kadhalika, magari yanayokwenda maeneo ya Vianzi Mkuranga, Malela, Pemba Mnazi, Mfuru njia zimefungwa kutokana na mapambano hayo.
=> Inadaiwa wamekamatwa majambazi 14 na wengi wao ni askari wastaafu. Kiongozi wa wahalifu wao anadaiwa kuwa Kanali wa Jeshi mstaafu.
No comments