Breaking News

27 Feb 2015 ZIARA YA WAZIRI MKUU PINDA MBEYA MJINI NA MBEYA VIJIJINI

5
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiweka jiwe la Msingi la zahanati ya Kimondo , Mbeya Vijijini akiwa katika ziara ya mkoa  wa Mbeya, Februari 25, 2015. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini Dr. Norman Sigalla.
4
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapungia wananchi wa Kijiji cha Kimondo, Mbeya Vijijini  kabla ya kuweka jiwe la Msingi la zahanati yao akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Februari 25, 2015. Kushoto kwake ni Mbunge wa Mbeya Vijijini, Luckson Mwanjale na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Mbeya mjini Dr. Norman Sigalla.
3
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua soko Kuu la Mjini Mbeya la Mwanjelwa baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wake akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya, Februari 25, 2015.
2
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwasikiliza wanafunzi wa shule ya sekondari ya Iwambe mjini Mbeya wakati alipofungua na kukagua maabara tatu za shule hiyo akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeaya Februari 25, 2015. Kushoto ni mkewe  Tunu. 
6
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wananchi baada ya kufungua vyumba vitatu vya Maabara katika shule ya sekondari ya Songwe mkoani Mbeya Febrari 25, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
9
Max Oswald (kushoto) na  Ivan Kina wakitumbuiza katika mkutano wa hadhara  uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika kijiji cha Igoma , Mbeya Vijijini Februari 25, 2015.
10

Wasanii Max Oswald ( Wapili Kulia) na  Ivan Kina  (wapili kushoto) wakisaidiwa kuvua nyasi walizokuwa wamejifunika kwa ajili ya kutoa burudani katika mkutano wa hadhara uliohutuibiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katia kijiji cha Igoma, Mbeya vijijini Februari 25, 2015.  Wanaowasaidia ni Oscar Ben (kulia) na Obadia Dandu

No comments